1 Yesu mwema mno, mlinzi wa viumbe,
Mwana wa mtu na wa Mungu
Nimwabudu Yesu, nim-sifu Bwana,
Mlinzi wa roho yangu.
2 Maua ni mema, hata na miti yote,
Na vimeavyo duniani,
Yezu huuzidi wema wa viumbe,
Hufurahisha rohoni.
3 Jua kitu chema, mwezi, nyota, usiku,
Na vyote vitaovyo nuru,
Nuru yake Yesu yazidi yo yote;
Huniangaza rohoni
Source: Nyimbo Za Imani Yetu #12